Wandishi wa habari walifika katika kijiji cha Mwigumbi kata ya Maganzo wilayani
Kishapu na kukutana na sakata hilo ambapo punde tu baada ya polisi
kuvamia eneo hilo wazazi wa watoto hao walikimbia na kujificha
pasipojulikana ndipo polisi walipowakamata vijana hao na kuwafikisha
katika kituo cha polisi cha Maganzo ambapo Msaidizi wa Kamanda wa Jeshi
la polisi mkoani Shinyanga Greyfton Mushi alithibitisha kutokea kwa
tukio hilo.
Aidha baadhi ya wakazi wa maeneo hayo walioshuhudia tukio hilo
walitoa maoni yao na kuiomba serikali kuwachukulia hatua kali wahusika
ili iwe fundisho kwa watu wenye tamaa ya kupata mali kwa kuozesha watoto
wadogo.
John Miyola ni Mkurugenzi wa shirika la Agape alimesema ndoa na mimba
za umri mdogo zinachangiwa na baadhi ya viongozi wa kata na vijiji
kushindwa kutambua wajibu wao katika jamii huku mkuu wa wilaya ya
Kishapu Bi.hawa Ng’humbi akiagiza watendaji hao pamoja na wazazi
wanaohusika kukamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kusheria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni