Jumatano, 4 Januari 2017

Mkuu Wa Jeshi La Polisi Nchini, Igp Ernest Mangu Atuma Timu Ya Maofisa Wa Jeshi La Polisi Kwenda Zanzibar Kuchunguza Vitendo Vya Udhalilishaji



Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu ametuma timu ya Maofisa  wa Polisi ikiongozwa na Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Alli Mussa kwenda Zanzibar kushughulikia kero na malalamiko ya wananchi juu ya vitendo vya udhalilishaji na ukatili kwa watoto/wanawake ambavyo vimekuwa vikiripotiwa mara kwa mara.

Timu hiyo imepewa jukumu la kuchunguza vitendo hivyo vya udhalilishaji na kiini chake na hatimaye kuja na mpango mkakati wa kuzuia vitendo hivyo ikiwemo kuwakamata  wahusika na kuwafikisha mahakamani.

IGP Mangu amewataka wananchi wa Zanzibar, Taasisi za kiserikali na Taasisi za kiraia zilizopo Zanzibar kutoa ushirikiano kwa timu hiyo ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya Watanzania.

Godbless Lema Arudishwa Tena Gerezani.....Ni Baada ya Serikali Kuwasilisha Notisi Ya Kupinga Dhamana yake Mahakama ya Rufaa



Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, leo imeshindwa kusikiliza rufani ya Jamhuri dhidi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kupinga dhamana yake, baada ya mawakili wa Serikali kuwasilisha notisi ya kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa wakipinga kusikilizwa kwa rufani hiyo .

Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Salma Maghimbi   alitarajiwa kutoa uamuzi juu ya rufaa ya Jamhuri iliyopinga  Lema kupatiwa dhamana Novemba 11 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Arusha, Desderi Kamugisha katika kesi namba 440 na 441/2016 ya kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli, ambapo siku hiyo Jamhuri iliwasilisha notisi ya mdomo.

Baada ya Lema kufikishwa mahakamani saa 3.25 asubuhi akiwa chini ya ulinzi mkali, huku pia polisi wakiwa wametanda viwanja vya Mahakama Kuu ndani na nje sanjari na gari moja la maji ya kuwasha, baada ya  mawakili wa pande zote kujitambulisha Jaji Maghimbi alisoma notisi ya Jamhuri kupeleka shauri hilo Mahakama ya Rufaa na kueleza kufungwa kisheria kutoa uamuzi wa rufani hiyo.

Anaswa na polisi akifukua kaburi la albino



Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia mtu mmoja kwa tuhuma za kufukua kaburi la marehemu ambaye likuwa ni mlemavu wa ngozi (Albino) aliyefariki mwaka 2010 kwa lengo la kuchukua viungo vyake.

Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa na Kamanda a Polisi Mkoani Mbeya DCP Dhahiri Kidavashari inasema kuwa mnamo tarehe 03.01.2017 majira ya saa 01:00 usiku katika Kijiji cha Mumba kilichopo Kata ya Ilembo, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JONAS JOHN mkazi wa Chapakazi alikamatwa na askari Polisi akiwa na wenzake wawili wakifukua kaburi la marehemu SISTER OSISARA aliyekuwa mlemavu wa ngozi (ALBINO)

Inadaiwa kuwa marehemu alifariki dunia mwaka 2010 kwa ugonjwa wa homa na kuzikwa katika makaburi ya Kijiji cha Mumba.

Mtuhumiwa alikutwa na majembe na makoleo ambayo walikuwa wakiyatumia kufukuria kaburi hilo. Baada ya mahojiano mtuhumwa huyo aliwataja washirika wenzake wawili ambao walikimbia baada ya kuwaona askari.

Jeshi hilo linaendelea na msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa .

Katika tukio lingine Mnamo tarehe 03.01.2017 majira ya saa 3:30 usiku katika kata ya Makongolosi wilayani Chunya, mkoa wa Mbeya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la KELVIN KUBANDA mkazi wa Kahama alikamatwa akiwa na bhangi kete 10 sawa na uzito wa gramu 55.

Mtuhumiwa alikamatwa akiwa katika kijiwe cha kuvutia Bhangi. Upelelezi unaendelea.

Jumanne, 3 Januari 2017

PIL Trade yaanzisha mafunzo kwa wafugaji kuku

Kampuni ya ufugaji na utengenezaji chakula cha kuku ya PIL Trade ya mjini DAR ES SALAAM imeanzisha shamba darasa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya ufugaji bora wa kuku kwa wajasiriamali

Kampuni ya ufugaji na utengenezaji chakula cha kuku ya PIL Trade ya mjini DAR ES SALAAM imeanzisha shamba darasa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya ufugaji bora wa kuku kwa wajasiriamali

 Akizungumza kwenye uzinduzi wa shamba hilo,mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Ismail Lankii amesema mafunzo hayo yatahusu utunzani wa kuku kuanzia vifaranga, uchangaji bora wa chakula na yatamwezesha mjasiriamali kuanzisha miradi ya kisasa ya ufugaji wa kuku.

Naye afisa masoko wa kampuni hiyo Sharifa Issah amewashauri  vijana kuanzisha miradi ya ufugaji wa kuku kwani ni njia ya uhakika ya kujipatia kipato.

TRA - ZANZIBAR yakusanya bilioni 80.17 kati ya mwezi Julai na Novemba

Mamlaka ya mapatoa nchini, TRA, ofisi ya ZANZIBAR imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 80.17 kwa kipindi cha kati ya mwezi Julai na Novemba 2016 kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato visiwani humo.

Mamlaka ya mapatoa nchini ,TRA - ofisi ya ZANZIBAR imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 80.17 kwa kipindi cha kati ya mwezi Julai na Novemba 2016 kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato visiwani humo.

Akizungumza mjini UNGUJA, naibu kamishna TRA Zanzibar , MCHA HASSAN MCHA amesema kiasi hicho cha mapato ni mwenendo mzuri wa makusanyo ambapo malengo ni kufikisha shilingi bilioni 188.80 utakapokamilika mwaka wa fedha wa 2016/17.

Shirika la manunuzi KARIAKOO lawatimua maafisa wake wa wili kwa manunuzi kinyume na taratibu

Shirika la masoko ya kariakoo limewasimamisha kazi maafisa wawili wa idara ya manunuzi kwa tuhuma za kufanya manunuzi kinyume cha sheria ya manunuzi.

Shirika la masoko ya Kariakoo limewasimamisha kazi maafisa wawili wa idara ya manunuzi kwa tuhuma za kufanya manunuzi kinyume cha sheria ya manunuzi.

Meneja Mkuu wa Shirika hilo HETSON KIPSI amewataja waliosimamishwa kazi ni mkuu wa kitengo cha manunuzi wa shirika hilo MATHIAS MBAFU  na msaidizi wake HENRIKA KAWILI .

KIPSI amesema maafisa hao wanatuhumiwa kughushi saini ya meneja mkuu ili waweze kununua mafuta ya jenereta na vifaa vingine na uchunguzi wa tuhuma hizo unaendelea.

GAMBO ataka kufuatiliwa fedha za mikopo ya wanawake na vijana


Mkuu wa mkoa wa ARUSHA, MRISHO GAMBO amemwagiza Mkuu wa wilaya ya ARUSHA kuunda timu ya kufuatilia fedha za mikopo zinazotolewa na halmashauri kwa ajili ya Vijana na Wanawake kwa kipindi cha miaka MITATU namna zilivyotumika.
 
Mkuu wa mkoa wa ARUSHA, MRISHO GAMBO amemwagiza Mkuu wa wilaya ya ARUSHA kuunda timu ya kufuatilia fedha za mikopo zinazotolewa na halmashauri kwa ajili ya Vijana na Wanawake kwa kipindi cha miaka MITATU namna zilivyotumika.

GAMBO ametoa agizo hilo jijini ARUSHA wakati akikabidhi mfano wahundi yenye thamani ya shilingi Milioni 425 kwa vikundi vya wanawake 85 na hundi ya shilingi Milioni 199 kwaajili ya vikundi 40 vya vijana wa jiji hilo,GAMBO nakusisitiza kuwa fedha hizo zinatakiwa zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa ya kufanya shughuli za kiujasiriamali.

 Amesema bado jiji hilo linatoa fedha kidogo ikilinganishwa na mapato yanayokusanywa na kuvinufaisha vikundi vya vijana na wanawake hivyo ni vyema mikopo iliyotolewa ikadhibitiwa ikiwa nipamoja na kufanya uchunguzi wa fedha za mikopo zilizotolewa katika kipindi cha miaka MITATU.

Kwa upande wake Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii katika jiji la ARUSHA, JANETH MMASI, amesema mikopo hiyo itasaidia vikundi 125 vya Vijana na Wanawake katika kujikwamua kiuchumi huku Mkuu wa wilaya ya ARUSHA, GABRIEL DAQQARO akiahidi kusimamia kikamilifu fedha hizo ili zitumike kama ilivyokusudiwa.